Kula ufuta paka mafta ya zaituni
Wednesday, February 19, 2014
Saturday, February 8, 2014
DAWA YA MAJERAHA NA VIDONDA SUGU
Tibu jeraha haraka na ondoa kovu sehemu hiyo ya jeraha kwa kufuata hatua zifuatazo;
Changanya na usage dhafarani ya unga na kaafuri kiasi cha kidonge kimoja cha kaafuri kwa vijiko viwili vya dhafarani
Weka maji jikoni yaache yachemke vizuri kisha yatowe jikoni hali ya kuwa umeyafunika yaache yapowe mpaka yawe vuguvugu. Osha sehemu yenye jeraha kwa maji hayo vuguvugu kisha weka kwa kunyunyiza kidogokidogo huo mchanganyiko wako wa kaafuri na dhafarani
Hakikisha kuwa umeweka sehemu yote ya donda, subiri kwa muda kidogo mpaka majimaji yakauke katika hilo jeraha kisha pakaa Asali mbichi sehemu ya juu ya jeraha lote, usilifunge jeraha lako liache wazi liwe linapitiwa na upepo, (Muhimu jeraha haliwezi kuadhiriwa na vijidudu likiwa limewekwa Asali,)
Fanya zoezi hilo asubuhi na jioni mpaka sehemu ya juu ya jeraha ifunge kwa kiwambo(ngozi laini yenye rangi nyekundu) hapo utaacha kutumia mchanganyiko wa kaafuri na asali, utakua unaosha kisha unapakaa maji ya Mti wa Aloe vera, unaacha kwa muda mpaka yakauke kisha unapakaa asali.
Endelea na zoezi hilo mpaka itakaporejea ngozi yako ya asili. Utarajibu huu wa tiba ya majeraha unatibu majeraha hata yale yaliyoisha sumbua kwa muda mrefu. Tiba hii hutibu majeraha ya aina zote.
Tafadhali usiondoke bila kuacha maoni yako na ushauri kwa ku comment hapo chini.
Tuesday, February 4, 2014
DAWA YA KUBATILISHA NZYONGO
Nzyongo ni aina ya uchawi unaotumiwa kuwadhuru watu kupitia macho,upepo na maji
kama umedhuriwa na nzyongo chukua majivu changanya na maji kisha jipakae mwili mzima zyomgo litaondoka mara nyingi zyongo ni michezo midogo midogo ya kichawi ikiwa halitoondoka basi litakua ni tatizo lingine.
kama umedhuriwa na nzyongo chukua majivu changanya na maji kisha jipakae mwili mzima zyomgo litaondoka mara nyingi zyongo ni michezo midogo midogo ya kichawi ikiwa halitoondoka basi litakua ni tatizo lingine.
Saturday, February 1, 2014
DAWA YA KUMFUKUZA JINI/SHETANI KATIAKA ENEO LAKO LA BIASHARA
Ukitaka kumfukuza jini katiaka eneo la biashara zako;1 Chukua mafuta ya kitunguu swaumu,2 mafuta ya karafuu kali,3 mafuta ya mnyonyo, 4 mafuta ya sidiri, 5 mafuta ya kasa (aina ya samaki mwenye kijungu cha mafuta), 6 mafuta ya zaituni, 7 mafuta ya habati soda yote kiasi cha robo lita
Yamimine mafuta yote hayo katiaka chungu, kisha changanya na dawa zifuatazo; 1 karafuu maiti 2 mvuje 3 miati saila 4 misk ya unga nyeusi 5 ambari 6 Unga wa mifupa ya samaki 7 mwanga jini
changanya vizuri dawa hizo katika hicho chungu cha mafuta kwa kukoroga
Weka jiko katiaka eneo lako la biashara, chemsha chungu hicho kikiwa wazi, acha kiendelee kuchemka kwa muda wa masaa 24 kwa siku ya kwanza, siku ya pili utachemsha kwa muda wa lisaa limoja kwa kuanzia saa ulio tolea kwa siku ya kwanza. Mfano; siku ya kwanza kama ulichemsha kwa kuanzia saa 1:00 asubuhi, utaitoa siku ya pili saa 1:00 asubuhi, siku hiyo ya pili utaiyacha, siku ya tatu utaichemsha kuanzia saa 1:00 hadi saa 2:00 siku ya tatu utaanzia saa 2:00 hadi saa 3:00 na utendelea na utaratibu huo kwa muda wa siku 7
Ukimaliza chungu hicho kakichimbie chini porini. tafadhali saana usikitupe hicho chungu sehemu yoyote,
Ukifanya kwa utaratibu huo jini ataondoka na kukimbia eneo hilo na hato rudi tena.
Tafadhali tunakuomba usiondoke bila kuacha maoni yako na ushsuri. pia mualike mwenzio ajitibu kupitia blog hii
DAWA YA KUZUIYA CHUMAULETE KATIKA BIASHARA
Kama unasumbuliwa na tatizo la kupoteza hela katika biashara katika hali isiyo ya kawaida. Unaweza ukafanya biashara yako vizuri lakini hela ukawa hauiyoni, fanaya mambo yafuatayo;
Chukua habbati soda iliyo sangwa vijiko 3 changanya na miski ya unga nusu ya kijiko. Toneshea matone ya mafuta ya sidiri huku ukiupuchua kwa mikono huo mchanganyiko wako wa dawa mpaka uhakikishe mchanganyiko wako wote uwe umeenea mafuta ya sidiri. Zingatia kuwa mchanganyiko wako inatakiwa uwe umeenea mafuta ya sidiri lakini uwe katika hali ya ukavu (vumbi)
Uweke mchanganyiko wako huo katika chupa ndogo ya kioo, funga mdomo wa chupa kisha livishe chupa lako kitambaa chenye rangi ya weusi au rangi nyekundu. Kalichimbie chupa lako na ulifukie sehemu ambayo kiasili hua haiyoti mimea au jaani (jalala la taka) au chini ya jiko la mafiga ya kuni, wakati wa usiku, liache hapo kwa muda wa siku saba kisha ulitoe na ulivue kitambaa, muda wa kulitoa ni lazima iwe mchana wakati jua lipo katikati ya dunia
Tumia dawa yako hiyo kwa kuirashia takita droo yako ya hela au sehemu unayo weka hela fanya zoezi hilo kila baada ya siku 7. Itunze dawa yako katiaka sehemu nzuri, epuka sehemu ambayo mwanamke anaweza akaishika akiwa katika hali ya hedhi.
Dawa hii inanguvu za ajabu za kuzuiya aina zote za chuma ulete.
Tafadhali usisome kisha ukaondoka bila ya kuacha maoni yako au ushauri. Mualike na mwenzio ajitibu kipitia blog hii.
Subscribe to:
Posts (Atom)